Binti yangu Anna.
Nina binti anaitwa Anna, amezaliwa tarehe 28, Februari (mwezi wa pili), mwaka 2008.Mimi na Anna tumetofautiana sana kitabia ;napenda paka,yeye mbwa,napenda mawe, yeye maua ,napenda kuvuta sigara na kujifunza kiswahili, yeye anapenda kucheza,kuimba,kuruka na kukimbia,napenda kulala, yeye hapendi,na mbaya zaidi si msikivu.
Anna ni binti mrembo mno, ana macho ya bluu na nywele nyeusi. Anasuka mitindo mbalimbali ya nywele, kila siku anabadili nguo,bangili na hereni,na anafurahi mno ninapomkubalia kupaka rangi ya mdomo. Ana kipaji kikubwa cha kucheza na kuimba muziki vizuri sana.
Walimu wake wanasisitiza anahitaji kujifunza kuimba muziki na kucheza, ili kuendeleza kipaji chake alichonacho. Tunaishi pamoja na mama yangu, anaitwa Nadezhda na ni daktari .Napenda familia yangu au ukoo wangu kuliko kitu chochote duniani.