zachariah getubo
Community-Tutor
JE WAJUA??

Wajua kwamba kuna tofauti kati ya maneno haya mawili>

Neno kuwa na neno kua>

Kuwa ni kitenzi kisaidizi, pia ni kitenzi cha silabi moja ambacho huongezwa silabi >KU  ili kuleta maana ya kutokea katika hali fulani au mahali fulani. Kwa mfano > Alikuwa darasani.

                                                 >Amekuwa akilima.

KUA ni kitenzi ambacho kinamaanisha > kuongezeka kwa binadamu katika kimo urefu na hata kunenepa.

Kwa mfano                           >Amekua mrefu.

                                                 >Amekua mnene.


2. Aug. 2018 08:01
Kommentare · 2
1
Asante kwa maelezo
8. August 2018
Karibu Malaika
8. August 2018